KUJIFUNGUA KWA OPERATION
KUJIFUNGUA KWA OPERATION
KARIBU sana ndugu msomaji wangu wa Afya muhimu Blog. Leo nakuletea makala inayo husu kujifungua kwa operation.
Siku hizi hasa kwa hapa taTanzan kumekuwa na wimbi kubwa la wanawake wengi kujifungua kwa njia ya operation na imekuwa kawaida kabisa kuliko hata kwa njia ya kawaida
Katika makala hii utapata kujifunza kuhusu
- Sababu za kujifungua kwa operation
- Madhara ya kujifungua kwa operation
- Njia za kuepuka kujifungua kwa operation.
Sasa soma hapa kwa makini.
SABABU ZA KUJIFUNGUA KWA OPERATION
Kuna sababu mbalimbali za kujifungua kwa operation ila zifuatazo ni kuu katika sababu hizo.
1. NJIA KUWA NDOGO.
Hii kwa akina mama wengi huwapata hasa kwa wale wenye maumbo madogo au wanawake wanene ambapo njia inakuwa ndogo kutokana na mafuta mengi mwilini na kupelekea kuubana uke na kushindwa kupitisha mtoto wakati wakutaka kujifungua.
2. UMRI.
Hii ni hasa kwa maeneo ya vijijini huwa inafanya kuwaua mabinti wengi wakati wa kujifungua. Inatokana na kuolewa wakiwa na umri mdogo ambapo njia ya uke huwa inakuwa ndogo na kushindwa kupitisha mtoto wakati wa kujifungua.
Ndio maana hii inapigwa vita Takriban ulimwengu mzima kwa kuepusha ndoa za utotoni.
3. MTOTO TUMBONI.
HAPA kuna sababu kuu mbili.
i.) Mtoto kukaa vibaya tumboni.
Mtoto kukaa vibaya tumboni ni ile hali ambapo mtoto badala ya kutanguliza kichwa basi inatangulia miguu. Hapa ni hakuna jinsi itabidi operation ihusike.
Mbeleni utapata kujua kwanini Mtoto anakaaa vibaya Tumboni.
ii.) Mtoto kuwa mkubwa.
Mtoto kuwa mkubwa inatokana na chakula ambacho alikuwa anakula mama wakati wa ujauzito wake hasa chakuwa chenye winyi wa fat(mafuta). Hii inamfanya mtoto kuwa mkubwa na kushindwa kupita katika njia ya uzazi.
4.) HORMONES
. (mfumo wa kemikali-taarifa za mwili)
Hormone inayohusika katika kujifungua mtoto inaitwa OXYTOCIN hii kwa wengi huita UCHUNGU . Hormone hii ikiharibiwa au ikiwa chini hupelekea kuwepo kwa uchungu mdogo au pengine kutowepo kwabisa na kupelekea operesheni.
5.) MTOTO KUFIA TUMBONI.
Mtoto kufia Tumboni hapa lazima operation itumike maana taarifa ya kujifungua huwa inatolewa na Mtoto mwenyewe akiwa tumboni kuwa Tayari Amesha kuwa na tayari kuanza maisha ya Dunia. Hivyo akiwa amefia TUMBONI hapo hamna namna nyingine.
MADHARA YA KUJIFUNGUA KWA
OPERATION
1.) KIFO (mama/mtoto)
Operation ikifanyika inaweza ikasababisha kifo aidha ni kwa mama au mtoto kama itafanyika vibaya.
Hivyo operation siyo jambo la kuzoea ni jambo la hatari.
2.) UPUNGUFU WA DAMU.
Wakati wa operation kunaweza kusababisha kupungukiwa kwa damu nyingi hii ni kwa mama anaye jifungua na muda mwingine hupelekea mtu Akafariki kutokana na upotevu mkubwa wa damu mwilini.
3.) MAAMBUKIZI YA MAGONJWA MENGINE.
KATIKA operation kumekuwa na maambukizo mengi sana ya magongwa hasa VVU/UKIMWI.
Hii inaweza kutokea maambukizi katika vifaa vya kufanyia operation, au maambukizi kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto endapo Damu ya mama na ya mtoto zikigusana. Hivyo huwa inahitaji umakini sana kama mama atajifungua kwa operation na pia kama ni Mwathirika wa VVU au UKIMWI.
JINSI YA KUEPUKA KUJIFUNGUA KWA
NJIA YA OPERATION
YAFUATAYO ni mambo mbalimbali ambayo umaweza zingazi wakati wa ujauzito ili kuepukana na Tatizo la kujifungua kwa operation.
1.) LISHE.
HAPA tunaongelea swala zima la Ulaji wa Mlo kamili. Hii hufanya kujengeka vizuri kwa mwili wa mama na mtoto na hata pia viungo vya uzazi kuwa imara na swala zima pia la UCHUNGU wakati wa kujifungua linakuwa La kawaida kwa sababu mwili unakuwa unazalisha UCHUNGU mwingi na kufanya kujifungua kwa njia ya kawaida na kwa haraka zaidi.
NB; EPUKA kula vyakula vyenye MAFUTA MENGI hasa pindi ujauzito utakapo fikia umri wa miezi SITA . Hii itapelekea kuuepusha mwili kuwa mkubwa ili isije leta swala la njia kuwa ndogo PIA inasaidia kutokunenepa kwa mtoto akiwa tumboni isije sababisha kushindwa kupita wakati wa kujifungua.
2.) EPUKA KUTUMIA MADAWA MBALIMBALI BILA YA USHAURI WA DAKTARI.
Wanawake wengi wamekuwa wakijisababishia kujikujif kwa operation kwa kisa cha kutumia madawa mbalimbali bila ya ushauri wa daktari.
Hasa wamekuwa wakitumia Dawa za kuondoa maumivu (Pain Killers) na bila kutambua viambata vyake katika utengenezaji wake. Hupelekea kupungua kwa Uchungu kwa sababu mwili unakuwa umehangaishwa na kemikali mbalimbali.
Pia kuna baadhi ya dawa hupelekea kutoka kwa mimba enyewe ( PLACENTAL DETACHMENT). Ndio Maana huwa Wanashauriwa kwenda Clinic wakati wa Ujauzito ili kujua Maendeleo ya Afya ya Mama na Mtoto.
3.) EPUKA KUTUMIA VINYWAJI VYA VIWANDANI.
Hapa sana sana tunaongelea Soda na baadhi ya vinywaji vingine ambavyo hupelekea kuongezeka kwa sumu mwilini na kufanya maendeleo mabaya ya mtoto akiwa tumboni.
Vinywaji vingine hufanya Mtoto kufariki akiwa Tumboni.
Unashauriwa ukiwa kama mama mjamzito pendelea matunda kwa wingi na mbogamboga ili kuupa mwili kinga na kuondoa sumu mwilini.
4.) EPUKA VITU VYENYE CAFFEINE NYINGI.
Hasa hii hupatikana kwenye vinywaji kama Kahawa, Cocacola, Energy drink n.k
Hii kwa mama mjamzito hatakiwi kabisa kutumia maana kwake yeye anaeza ona ni sawa lakini madhara makubwa yanampata mtoto maana hupelekea mzunguko mkubwa wa damu na mapigo ya moyo yakienda kasi hufanya mtoto akafariki.
5.) EPUKA MATUMIZI YA VILEVI VYOVYOTE.
Vilevi kama sigara, pombe na madawa ya kulevya hupelekea kusababisha kifo kwa mtoto au pia kupungukiwa kwa nguvu za kujifungua sababu ya uchungu mdogo ulio haribiwa na matumizi ya vilevi.
6.) MUONE DAKTARI MARA KWA MARA UKIWA MJAMZITO.
Kama ukizingatia haya hutaweza kujifungua kwa operation.
KARIBU sana ndugu msomaji wangu wa Afya muhimu Blog. Leo nakuletea makala inayo husu kujifungua kwa operation.
Siku hizi hasa kwa hapa taTanzan kumekuwa na wimbi kubwa la wanawake wengi kujifungua kwa njia ya operation na imekuwa kawaida kabisa kuliko hata kwa njia ya kawaida
Katika makala hii utapata kujifunza kuhusu
- Sababu za kujifungua kwa operation
- Madhara ya kujifungua kwa operation
- Njia za kuepuka kujifungua kwa operation.
Sasa soma hapa kwa makini.
SABABU ZA KUJIFUNGUA KWA OPERATION
Kuna sababu mbalimbali za kujifungua kwa operation ila zifuatazo ni kuu katika sababu hizo.
1. NJIA KUWA NDOGO.
Hii kwa akina mama wengi huwapata hasa kwa wale wenye maumbo madogo au wanawake wanene ambapo njia inakuwa ndogo kutokana na mafuta mengi mwilini na kupelekea kuubana uke na kushindwa kupitisha mtoto wakati wakutaka kujifungua.
2. UMRI.
Hii ni hasa kwa maeneo ya vijijini huwa inafanya kuwaua mabinti wengi wakati wa kujifungua. Inatokana na kuolewa wakiwa na umri mdogo ambapo njia ya uke huwa inakuwa ndogo na kushindwa kupitisha mtoto wakati wa kujifungua.
Ndio maana hii inapigwa vita Takriban ulimwengu mzima kwa kuepusha ndoa za utotoni.
3. MTOTO TUMBONI.
HAPA kuna sababu kuu mbili.
i.) Mtoto kukaa vibaya tumboni.
Mtoto kukaa vibaya tumboni ni ile hali ambapo mtoto badala ya kutanguliza kichwa basi inatangulia miguu. Hapa ni hakuna jinsi itabidi operation ihusike.
Mbeleni utapata kujua kwanini Mtoto anakaaa vibaya Tumboni.
ii.) Mtoto kuwa mkubwa.
Mtoto kuwa mkubwa inatokana na chakula ambacho alikuwa anakula mama wakati wa ujauzito wake hasa chakuwa chenye winyi wa fat(mafuta). Hii inamfanya mtoto kuwa mkubwa na kushindwa kupita katika njia ya uzazi.
4.) HORMONES
. (mfumo wa kemikali-taarifa za mwili)
Hormone inayohusika katika kujifungua mtoto inaitwa OXYTOCIN hii kwa wengi huita UCHUNGU . Hormone hii ikiharibiwa au ikiwa chini hupelekea kuwepo kwa uchungu mdogo au pengine kutowepo kwabisa na kupelekea operesheni.
5.) MTOTO KUFIA TUMBONI.
Mtoto kufia Tumboni hapa lazima operation itumike maana taarifa ya kujifungua huwa inatolewa na Mtoto mwenyewe akiwa tumboni kuwa Tayari Amesha kuwa na tayari kuanza maisha ya Dunia. Hivyo akiwa amefia TUMBONI hapo hamna namna nyingine.
MADHARA YA KUJIFUNGUA KWA
OPERATION
1.) KIFO (mama/mtoto)
Operation ikifanyika inaweza ikasababisha kifo aidha ni kwa mama au mtoto kama itafanyika vibaya.
Hivyo operation siyo jambo la kuzoea ni jambo la hatari.
2.) UPUNGUFU WA DAMU.
Wakati wa operation kunaweza kusababisha kupungukiwa kwa damu nyingi hii ni kwa mama anaye jifungua na muda mwingine hupelekea mtu Akafariki kutokana na upotevu mkubwa wa damu mwilini.
3.) MAAMBUKIZI YA MAGONJWA MENGINE.
KATIKA operation kumekuwa na maambukizo mengi sana ya magongwa hasa VVU/UKIMWI.
Hii inaweza kutokea maambukizi katika vifaa vya kufanyia operation, au maambukizi kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto endapo Damu ya mama na ya mtoto zikigusana. Hivyo huwa inahitaji umakini sana kama mama atajifungua kwa operation na pia kama ni Mwathirika wa VVU au UKIMWI.
JINSI YA KUEPUKA KUJIFUNGUA KWA
NJIA YA OPERATION
YAFUATAYO ni mambo mbalimbali ambayo umaweza zingazi wakati wa ujauzito ili kuepukana na Tatizo la kujifungua kwa operation.
1.) LISHE.
HAPA tunaongelea swala zima la Ulaji wa Mlo kamili. Hii hufanya kujengeka vizuri kwa mwili wa mama na mtoto na hata pia viungo vya uzazi kuwa imara na swala zima pia la UCHUNGU wakati wa kujifungua linakuwa La kawaida kwa sababu mwili unakuwa unazalisha UCHUNGU mwingi na kufanya kujifungua kwa njia ya kawaida na kwa haraka zaidi.
NB; EPUKA kula vyakula vyenye MAFUTA MENGI hasa pindi ujauzito utakapo fikia umri wa miezi SITA . Hii itapelekea kuuepusha mwili kuwa mkubwa ili isije leta swala la njia kuwa ndogo PIA inasaidia kutokunenepa kwa mtoto akiwa tumboni isije sababisha kushindwa kupita wakati wa kujifungua.
2.) EPUKA KUTUMIA MADAWA MBALIMBALI BILA YA USHAURI WA DAKTARI.
Wanawake wengi wamekuwa wakijisababishia kujikujif kwa operation kwa kisa cha kutumia madawa mbalimbali bila ya ushauri wa daktari.
Hasa wamekuwa wakitumia Dawa za kuondoa maumivu (Pain Killers) na bila kutambua viambata vyake katika utengenezaji wake. Hupelekea kupungua kwa Uchungu kwa sababu mwili unakuwa umehangaishwa na kemikali mbalimbali.
Pia kuna baadhi ya dawa hupelekea kutoka kwa mimba enyewe ( PLACENTAL DETACHMENT). Ndio Maana huwa Wanashauriwa kwenda Clinic wakati wa Ujauzito ili kujua Maendeleo ya Afya ya Mama na Mtoto.
3.) EPUKA KUTUMIA VINYWAJI VYA VIWANDANI.
Hapa sana sana tunaongelea Soda na baadhi ya vinywaji vingine ambavyo hupelekea kuongezeka kwa sumu mwilini na kufanya maendeleo mabaya ya mtoto akiwa tumboni.
Vinywaji vingine hufanya Mtoto kufariki akiwa Tumboni.
Unashauriwa ukiwa kama mama mjamzito pendelea matunda kwa wingi na mbogamboga ili kuupa mwili kinga na kuondoa sumu mwilini.
4.) EPUKA VITU VYENYE CAFFEINE NYINGI.
Hasa hii hupatikana kwenye vinywaji kama Kahawa, Cocacola, Energy drink n.k
Hii kwa mama mjamzito hatakiwi kabisa kutumia maana kwake yeye anaeza ona ni sawa lakini madhara makubwa yanampata mtoto maana hupelekea mzunguko mkubwa wa damu na mapigo ya moyo yakienda kasi hufanya mtoto akafariki.
5.) EPUKA MATUMIZI YA VILEVI VYOVYOTE.
Vilevi kama sigara, pombe na madawa ya kulevya hupelekea kusababisha kifo kwa mtoto au pia kupungukiwa kwa nguvu za kujifungua sababu ya uchungu mdogo ulio haribiwa na matumizi ya vilevi.
6.) MUONE DAKTARI MARA KWA MARA UKIWA MJAMZITO.
Kama ukizingatia haya hutaweza kujifungua kwa operation.
Comments
Post a Comment