KUTOKWA NA HARUFU MBAYA MDOMONI
KUTOA HARUFU MBAYA MDOMONI.
Kutokwa na harufu mbaya mdomoni ni moja ya tatizo ambayo baadhi ya watu katika jamii hupata na kuwafanya upweke kutokana na adha hiyo.
SABABU YA KUTOKWA NA HARUFU MBAYA MDOMONI.
Kuna sababu mbalimbali zinazo sababisha mtu kutokwa na harufu mbaya mdomoni Lakini sababu kuu ni FANGASI.
1. Fangasi.
Faghasi kwa kawaida huwa ikiwepo sehemu yoyote ya mwili hufanya sehemu hiyo kutoa harufu mbaya.
Basi fangasi hii ikikaa katika mdomo kwenye Fizi, Meno au ulimi hufanya kutuka kwa harufu mbaya mdomoni ambayo hata mtu akiswaki mara nyingi au kusukutua bado itakuwa haisaidii kitu.
2. Kutosafisha kinywa mara kwa mara.
Kusafisha kinywa mara kwa mara husaidia kuondoa mabaki ya chakula ambayo yakikaa kwa muda mrefu kwenye kinywa basi husababisha kutokwa kwa harufu.
3. Kula vitu vinavyo weza kutoa harufu kali kinywani.
Ulaji wa vitu kama vitunguu maji au saumu hasa vikiwa vibichi, Kabichi mbichi, samaki n.k husababisha kinywa kutoa harufu.
MADHARA YA KUTOKWA NA HARUFU MBAYA KINYWANI.
Madhara ya kutokwa na harufu mbaya kinywani ni kama ifuatavyo:
- Kutengwa na watu.
Hii huathiri sana saikolojia ya mtu binafsi na kujikuta mpweke sana kwa kuwa watu humwepuka kutokana na harufu kali ambayo anatoa kinywani.
- Kichefuchefu.
Harufu mbaya kinywani husababisha muda mwingine mtu kujihisi kichefuchefu na mwingine hadi kutapika kutokana na harufu kumkera.
- Kuharibu mahusiano hasa kwa wapenzi.
Harufu mbaya kinywani hupelekea kuvunja mahusiano ya kimapenzi kutokana na mmoja wapo kushindwa kuwa na mwenzake kutokana na harufu kali anayo toa kinywani.
- Kutokujiamini.
Mtu mwenye tatizo hili huwa hawezi kujiamini hasa anapokuwa na watu na anapotaka kuzungumza na mtu kwa kuhofia kusikika kwa harufu kali anayo toa kinywani.
Hii pia huwafanya hata vijana wengi walio na tatizo hili kushindwa kujiingiza katika mahusiano ya kimapenza kwa kuhofia tatizo lake.
NAMNA YA KUEPUKANA NA TATIZO HILI.
ILI uweze kuepukana na tatizo hili basi fanya yafuatayo:
- Safisha kinywa mara kwa mara hasa kwa kutumia chumvi au ndimu ambayo inasaidia kusafisha sehemu zote zenye michubuko ambazo zinaweza kupelekea kukua kwa fangasi.
- Kila baada ya mlo wako wowote sukutua kwa maji safi ili kuzuia mabaki ya chakula kuganda kwenye meno au fizi.
- Safisha ulimi kwa maji na dawa ya meno. Watu wengi huwa wanasahau kusafisha ulimi lakini pia ndicho chanzo cha harufu kinywani.
- Tumia dawa zinazo ondoa fangasi kinywani.
- Epuka ulaji wa vitu vinavyo acha harufu mbaya kinywani. Kama vutunguu na kama utatumia basi safisha kinywa ili usibaki na harufu hiyo.
#Kama tatizo litazidi basi nenda kwenye kituo cha afya onana na mtaalamu wa kinywa na meno.
All the best in your health
-
Kutokwa na harufu mbaya mdomoni ni moja ya tatizo ambayo baadhi ya watu katika jamii hupata na kuwafanya upweke kutokana na adha hiyo.
SABABU YA KUTOKWA NA HARUFU MBAYA MDOMONI.
Kuna sababu mbalimbali zinazo sababisha mtu kutokwa na harufu mbaya mdomoni Lakini sababu kuu ni FANGASI.
1. Fangasi.
Faghasi kwa kawaida huwa ikiwepo sehemu yoyote ya mwili hufanya sehemu hiyo kutoa harufu mbaya.
Basi fangasi hii ikikaa katika mdomo kwenye Fizi, Meno au ulimi hufanya kutuka kwa harufu mbaya mdomoni ambayo hata mtu akiswaki mara nyingi au kusukutua bado itakuwa haisaidii kitu.
2. Kutosafisha kinywa mara kwa mara.
Kusafisha kinywa mara kwa mara husaidia kuondoa mabaki ya chakula ambayo yakikaa kwa muda mrefu kwenye kinywa basi husababisha kutokwa kwa harufu.
3. Kula vitu vinavyo weza kutoa harufu kali kinywani.
Ulaji wa vitu kama vitunguu maji au saumu hasa vikiwa vibichi, Kabichi mbichi, samaki n.k husababisha kinywa kutoa harufu.
MADHARA YA KUTOKWA NA HARUFU MBAYA KINYWANI.
Madhara ya kutokwa na harufu mbaya kinywani ni kama ifuatavyo:
- Kutengwa na watu.
Hii huathiri sana saikolojia ya mtu binafsi na kujikuta mpweke sana kwa kuwa watu humwepuka kutokana na harufu kali ambayo anatoa kinywani.
- Kichefuchefu.
Harufu mbaya kinywani husababisha muda mwingine mtu kujihisi kichefuchefu na mwingine hadi kutapika kutokana na harufu kumkera.
- Kuharibu mahusiano hasa kwa wapenzi.
Harufu mbaya kinywani hupelekea kuvunja mahusiano ya kimapenzi kutokana na mmoja wapo kushindwa kuwa na mwenzake kutokana na harufu kali anayo toa kinywani.
- Kutokujiamini.
Mtu mwenye tatizo hili huwa hawezi kujiamini hasa anapokuwa na watu na anapotaka kuzungumza na mtu kwa kuhofia kusikika kwa harufu kali anayo toa kinywani.
Hii pia huwafanya hata vijana wengi walio na tatizo hili kushindwa kujiingiza katika mahusiano ya kimapenza kwa kuhofia tatizo lake.
NAMNA YA KUEPUKANA NA TATIZO HILI.
ILI uweze kuepukana na tatizo hili basi fanya yafuatayo:
- Safisha kinywa mara kwa mara hasa kwa kutumia chumvi au ndimu ambayo inasaidia kusafisha sehemu zote zenye michubuko ambazo zinaweza kupelekea kukua kwa fangasi.
- Kila baada ya mlo wako wowote sukutua kwa maji safi ili kuzuia mabaki ya chakula kuganda kwenye meno au fizi.
- Safisha ulimi kwa maji na dawa ya meno. Watu wengi huwa wanasahau kusafisha ulimi lakini pia ndicho chanzo cha harufu kinywani.
- Tumia dawa zinazo ondoa fangasi kinywani.
- Epuka ulaji wa vitu vinavyo acha harufu mbaya kinywani. Kama vutunguu na kama utatumia basi safisha kinywa ili usibaki na harufu hiyo.
#Kama tatizo litazidi basi nenda kwenye kituo cha afya onana na mtaalamu wa kinywa na meno.
All the best in your health
-
Comments
Post a Comment